Muslim Library

Surah Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud)

Swahili

Surah Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) - Aya count 36
Facebook Twitter Google+ Pinterest Reddit StumbleUpon Linkedin Tumblr Google Bookmarks Email
وَيْلٌ لِّلْمُطَفِّفِينَ ( 1 ) Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) - Aya 1
Ole wao hao wapunjao!
الَّذِينَ إِذَا اكْتَالُوا عَلَى النَّاسِ يَسْتَوْفُونَ ( 2 ) Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) - Aya 2
Ambao wanapo jipimia kwa watu hudai watimiziwe.
وَإِذَا كَالُوهُمْ أَو وَّزَنُوهُمْ يُخْسِرُونَ ( 3 ) Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) - Aya 3
Na wao wanapo wapimia watu kwa kipimo au mizani hupunguza.
أَلَا يَظُنُّ أُولَٰئِكَ أَنَّهُم مَّبْعُوثُونَ ( 4 ) Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) - Aya 4
Kwani hawadhani hao kwamba watafufuliwa
لِيَوْمٍ عَظِيمٍ ( 5 ) Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) - Aya 5
Katika Siku iliyo kuu,
يَوْمَ يَقُومُ النَّاسُ لِرَبِّ الْعَالَمِينَ ( 6 ) Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) - Aya 6
Siku watapo msimamia watu Mola Mlezi wa walimwengu wote?
كَلَّا إِنَّ كِتَابَ الْفُجَّارِ لَفِي سِجِّينٍ ( 7 ) Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) - Aya 7
Hasha! Hakika maandiko ya wakosefu bila ya shaka yamo katika Sijjin.
وَمَا أَدْرَاكَ مَا سِجِّينٌ ( 8 ) Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) - Aya 8
Unajua nini Sijjin?
كِتَابٌ مَّرْقُومٌ ( 9 ) Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) - Aya 9
Kitabu kilicho andikwa.
وَيْلٌ يَوْمَئِذٍ لِّلْمُكَذِّبِينَ ( 10 ) Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) - Aya 10
Ole wao siku hiyo kwa wanao kadhibisha!
الَّذِينَ يُكَذِّبُونَ بِيَوْمِ الدِّينِ ( 11 ) Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) - Aya 11
Ambao wanaikadhibisha Siku ya Malipo.
وَمَا يُكَذِّبُ بِهِ إِلَّا كُلُّ مُعْتَدٍ أَثِيمٍ ( 12 ) Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) - Aya 12
Wala haikadhibishi ila kila mwenye kuruka mipaka, mwenye dhambi.
إِذَا تُتْلَىٰ عَلَيْهِ آيَاتُنَا قَالَ أَسَاطِيرُ الْأَوَّلِينَ ( 13 ) Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) - Aya 13
Anapo somewa Aya zetu husema: Ni visa vya watu wa kale!
كَلَّا ۖ بَلْ ۜ رَانَ عَلَىٰ قُلُوبِهِم مَّا كَانُوا يَكْسِبُونَ ( 14 ) Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) - Aya 14
Hasha! Bali yametia kutu juu ya nyoyo zao hao walio kuwa wakiyachuma.
كَلَّا إِنَّهُمْ عَن رَّبِّهِمْ يَوْمَئِذٍ لَّمَحْجُوبُونَ ( 15 ) Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) - Aya 15
Hasha! Hakika hao siku hiyo bila ya shaka watazuiliwa na neema za Mola wao Mlezi.
ثُمَّ إِنَّهُمْ لَصَالُو الْجَحِيمِ ( 16 ) Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) - Aya 16
Kisha wataingia Motoni!
ثُمَّ يُقَالُ هَٰذَا الَّذِي كُنتُم بِهِ تُكَذِّبُونَ ( 17 ) Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) - Aya 17
Kisha waambiwe: Haya ndiyo mliyo kuwa mkiyakadhabisha.
كَلَّا إِنَّ كِتَابَ الْأَبْرَارِ لَفِي عِلِّيِّينَ ( 18 ) Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) - Aya 18
Hasha! Hakika maandiko ya watu wema bila ya shaka yamo katika I'liyyin.
وَمَا أَدْرَاكَ مَا عِلِّيُّونَ ( 19 ) Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) - Aya 19
Na nini kitakacho kujuvya nini I'liyyin?
كِتَابٌ مَّرْقُومٌ ( 20 ) Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) - Aya 20
Kitabu kilicho andikwa.
يَشْهَدُهُ الْمُقَرَّبُونَ ( 21 ) Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) - Aya 21
Wanakishuhudia walio karibishwa.
إِنَّ الْأَبْرَارَ لَفِي نَعِيمٍ ( 22 ) Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) - Aya 22
Hakika watu wema bila ya shaka watakuwa katika neema.
عَلَى الْأَرَائِكِ يَنظُرُونَ ( 23 ) Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) - Aya 23
Wakae juu ya viti vya enzi wakiangalia.
تَعْرِفُ فِي وُجُوهِهِمْ نَضْرَةَ النَّعِيمِ ( 24 ) Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) - Aya 24
Utatambua katika nyuso zao mng'aro wa neema,
يُسْقَوْنَ مِن رَّحِيقٍ مَّخْتُومٍ ( 25 ) Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) - Aya 25
Watanyweshwa kinywaji safi kiliyo tiwa muhuri,
خِتَامُهُ مِسْكٌ ۚ وَفِي ذَٰلِكَ فَلْيَتَنَافَسِ الْمُتَنَافِسُونَ ( 26 ) Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) - Aya 26
Muhuri wake ni miski. Na katika hayo washindanie wenye kushindana.
وَمِزَاجُهُ مِن تَسْنِيمٍ ( 27 ) Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) - Aya 27
Na mchanganyiko wake ni Tasniim,
عَيْنًا يَشْرَبُ بِهَا الْمُقَرَّبُونَ ( 28 ) Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) - Aya 28
Chemchem watakayo inywa walio kurubishwa.
إِنَّ الَّذِينَ أَجْرَمُوا كَانُوا مِنَ الَّذِينَ آمَنُوا يَضْحَكُونَ ( 29 ) Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) - Aya 29
Kwa hakika wale walio kuwa wakosefu walikuwa wakiwacheka walio amini.
وَإِذَا مَرُّوا بِهِمْ يَتَغَامَزُونَ ( 30 ) Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) - Aya 30
Na wanapo pita karibu yao wakikonyezana.
وَإِذَا انقَلَبُوا إِلَىٰ أَهْلِهِمُ انقَلَبُوا فَكِهِينَ ( 31 ) Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) - Aya 31
Na wanapo rudi kwa watu wao hurudi nao wamefurahi.
وَإِذَا رَأَوْهُمْ قَالُوا إِنَّ هَٰؤُلَاءِ لَضَالُّونَ ( 32 ) Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) - Aya 32
Na wanapo waona husema: Hakika hawa ndio khasa walio potea.
وَمَا أُرْسِلُوا عَلَيْهِمْ حَافِظِينَ ( 33 ) Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) - Aya 33
Na wao hawakutumwa wawe walinzi juu yao.
فَالْيَوْمَ الَّذِينَ آمَنُوا مِنَ الْكُفَّارِ يَضْحَكُونَ ( 34 ) Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) - Aya 34
Basi leo walio amini ndio watawacheka makafiri,
عَلَى الْأَرَائِكِ يَنظُرُونَ ( 35 ) Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) - Aya 35
Nao wako juu ya viti vya enzi wakiangalia.
هَلْ ثُوِّبَ الْكُفَّارُ مَا كَانُوا يَفْعَلُونَ ( 36 ) Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) - Aya 36
Je! makafiri wamelipwa malipo ya yale waliyo kuwa wakiyatenda?
Facebook Twitter Google+ Pinterest Reddit StumbleUpon Linkedin Tumblr Google Bookmarks Email

Select language

Select surah